MAHAKAMA
 Kuu Kanda ya Dodoma imefutilia mbali kesi ya uchaguzi iliyofunguliwa na
 mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Jonathan Njau kupinga ushindi wa 
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu (CHADEMA).
Katika madai yake ya msingi, Njau alikuwa akipinga matokeo na kutaka kura kuhesabiwa upya.
Shauri
 hilo lilikuwa mbele ya Jaji Berkel Sehel ambapo mgombea wa ubunge 
kupitia chama cha Mapinduzi CCM Jonathan Njau alishindwa kwenye uchaguzi
 kwenye jimbo hilo mwaka 2010 na 2015.
Njau Aliwasilisha ombi mahakamani la kutaka kesi hiyo kufutwa kwani hana haja ya kuendelea na shauri hilo.
Awali
 mlalamikaji aliwahi kupeleka mahakamani mara mbili maombi ya ombi la 
kusamehewa kwa gharama za kesi kiasi cha milioni 15 lakini maombi hayo 
yalitupwa
Lisu amesema Mahakama kuu ilishatamka mwaka 2010 kuwa kesi za uchaguzi si za kuendea kwa papara bila umakini wowote.
 
No comments:
Post a Comment