Aliyekuwa
 Waziri wa Kilimo na Chakula na Kada mkongwe wa Chama Cha Mapinduzi 
(CCM), Stephen Wassira ameomba wasaidizi wa Rais John Magufuli kumshauri
 kufanya mazungumzo na viongozi wa upinzani ili kuepusha madhara 
yanayoweza  kutokea kutokana na maandamano yanayopangwa kufanyika 
Septemba 1.
Wassira
 ameeleza kuwa washauri hao wanapaswa kufanya hivyo kwani bado nafasi 
hiyo ipo kuliko kuacha Rais aingie vitani na wananchi wake kwani madhara
 yatawapata Watanzania wote.
“Wazungumze
 ili wasimuingize Rais kupigana na watu wake kwa maana wote tutapoteza. 
Kwa nini uweke askari polisi wote hao, msimweke Rais kwenye vita na watu
 wake,” Wassira anakaririwa na Jambo Leo.
“Kinachohitajika
 ni wasaidizi wa Rais kumshauri ili kuhakikisha kuwa tofuati zilizopo 
baina yake na vyama vya upinzani haziendelei ili kuepusha madhara 
yanayoweza kuzuilika, itafutwe suluhu,” aliongeza.
Akizungumzia
 uamuzi wa Serikali kupiga marufuku kufanyika kwa mikutano na 
maandamano, alisema kuwa tatizo linaweza kuwa ni aliyekuwa Mgombea wa 
Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa.
Alisema
 kuwa hii inatokana na joto la uchaguzi lililokuwepo pamoja na nia ya 
Lowassa kuzunguka nchi nzima kuwashukuru wapiga kura, kungeweza kuzua 
tafrani kubwa kwani alipata kura nyingi na alikuwa akidai ameshinda kwa 
asilimia 62.
“Ukiwaruhusu
 kufanya mikutano na ukwaambia kuwa atakayekuja kutoa shukurani ni 
Lowassa, ambaye amekuwa akipinga kushindwa ni sawa na kurejesha hali ya 
uchaguzi kipindi hiki,” alisema.
Alitaka Serikali kutoa elimu ya wazi kwa umma kuhusu sababu zinazopelekea kukataza kufanyika kwa mikutano ili kuweka mambo sawa.
“Kama
 mimi hapa nimetaja sababu kwamba inawezakana kuwa ni Lowassa. Sasa na 
wao Serikali waseme tu tunapiga marufuku mikutano na maandamano… wataje 
[sababu]na kuzifafanua,” alieleza.
Hata
 hivyo, Wassira aliwataka Chadema kusitisha adhma yao na kuhakikisha 
wanafuata utaratibu ili kupata haki ya kufanya maandamano na mikutano 
ambayo alieleza kuwa kila Katiba ya nchi duniani imeiweka, lakini bila 
kufuata utaratibu haiwezi kuruhusiwa.

 
No comments:
Post a Comment