Saturday, December 12, 2015

Fredrick Sumaye Atangaza Rasmi kuwa Mwanachama wa Chadema.


Mpekuzi blog
  
Waziri  mkuu wa awamu ya tatu Mh.Fredirick Sumaye jana alitangaza  rasmi kujiunga na chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) na  akakabidhiwa kadi na Mwenyekiti  wa chama hicho Mh.Freeman  Mbowe.
 
Sumaye ambaye wakati wa uchaguzi alitangaza kujiondoa  CCM na  kudai  kuwa  anaunga mkono  mageuzi yanayofanywa na vyama  vinavyounda  katiba  ya  wananchi (UKAWA) bila  kuweka  wazi  kuwa yuko kwenye chama kipi  kati ya  hivyo amesema sasa ameamua  kujiunga na CHADEMA.

Akizungumza katika mkutano wa kufunga kampeni za ubunge wa  jimbo la Arusha  kwa chama cha CHADEMA uliofanyika kata ya Baraa, Sumaye  alisema anataka  kuungana na wanamageuzi wenzake katika  kuendeleza  harakati za mabadiliko hapa nchini ambazo bado  zinaendelea.

Akizungumza  baada ya kumkabidhi kadi Mwenyekiti wa chama hicho  Mh.Freeman Mbowe alisema chadema na vyama washirika wa  UKAWA bado viko imara na vimeendelea kuimarika na kwamba licha ya kudhulumiwa ushindi  azma yao ya  kuleta ukombozi  nchini iko  pale pale.

Awali aliyekluwa  mgombea uras wa CHADEMA akiwakilisha vyama vya umoja wa katiba ya wananchi ukawa Mh.Edward Lowassa ameendelea kuwataka watanzania wanaounga mkono mabadiliko kuwa watulivu na kwamba kwa vile wana dhamira ya dhati ya kuyaona mabadiliko hakuna kukata tamaa kwani bado kuna fursa yakufikiwa   kwa malengo yao

No comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments system